|
Sheikh Muhammad Sayyid Tantawi afariki dunia

إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا
إِلَيْهِ رَاجِعونَ


Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh I ssa
Shaabani Simba (shoto) akiwa katika picha ya pamoja na Sheikh Mkuu wa
Misri (Sheikhul-Azhar - GRAND SHEIKH OF AL-AZHAR - Pr,) Dr Muhammad
Sayyid Tantawi katika Ofisi yake mwezi uliopita.

Sheikh Mkuu wa Tanzania alikuwa nchini
Misri kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 22 (The 22nd General Conference. Under
the Title The Objectives of Shariah (Islamic Law) And Issues of the
Contemporary Age.
Marehemu amefariki Jumatano ya tarehe
10/03/2010 (24 Raby' Al-Awwal 1431 A.H.) asubuhi katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Riadh
nchini Saudi Arabia akijiaanda kwa safari ya kurudi nchini Misri. Mara
baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo, Sheikh alikimbizwa katika hospitali
ya King Khaled military hospital ambapo alipofariki dunia.
Sheikh
alikuwa nchini Saudia Arabia kuhudhuria hafla ya ugawaji wa tunzo ya
Mfalme Faisal iliyokuwa ikigaiwa kwa baadhi ya viongozi kutoka nchi
mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu wa Uturuki.
Sababu za kifo chake ni Presha (Mshtuko wa
Moyo) uliomtokea ghafla akiwa kwenye ngazi ya ndege. Taarifa zinasema
hali hiyo imetokana na uchovu aliopata kutokana na shughuli hiyo ya jana.
اللهم اغفر له وارحمه

Zingatia: hakikisha
kompyuta yako ina 'support' maandishi ya kiarabu kwa kusoma
maandishi yaliyoandikwa kwa kiarabu kwenye website hii.
|